Na Mwandishi Wetu
TAASISI
 ya Wanawake na Diplomasia, imetoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Dk.Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoendelea 
kutumia diplomasia kuifungua nchini katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya 
uchumi na diplomasia.
Akizungumza leo  jijini Dar es Salaam 
kwenye Kongamano maalum lililoandaliwa na Taasisi ya Wanawake na 
Diplomasia na kuhusisha mabalozi, wanadiplomasia kutoka taasisi na 
kampuni mbalimbali, Mwanadiplomasia mkongwe Balozi Liberata Mulamula 
ametumia nafasi hiyo kuelezea namna ambavyo Rais Samia amekuwa kinara wa
 diplomasia.
“Diplomasia inatumika katika mambo mengi yakiwemo 
kuangalia jinsi gani mnaweza kutatua mifarakano, matatizo kwa njia za 
mazungumzo, kwa njia zuri na huenda wanawake tumezaliwa na huo ujuzi ,  
nimefarikijika kwani mwaka jana taasisi hii ilipotukutanisha kulikuwa na
 wanawake kutoka Serikalini.
“Wanawake wanaojulikana sana lakini 
leo tumekuwa na wanawake ambao wametoka kwenye eneo la biashara na 
tunafahamu hata katika kufanya bashara unatumia diplomasia katika 
kuvutia biashara yako.Hivyo wakati leo tuaadhimishi siku ya wanawake 
duniani hawa vijana wameamua tuwe na siku maalumu.
“Kwani huwa 
tumekuwa tunazungumzia, wanawake katika siasa, wanawake katika biashara 
lakini leo hii ni wanawake katika diplomasia mimi mnajua ni kama 
nilizaliwa kwenye diplomasia, nimezeeka kwenye diplomasia lakini hawa 
vijana wamechukua jukumu la kuhakikisha nchi yetu inaendelea kuzalisha 
wana diplomasia,”amesema Balozi Mulamula.
Aidha amesema Tanzania 
kwenye eneo la diplomasia iko vizuri na ndio maana haina nchi adui , 
hiyo inatokana na kazi kubwa iliyofanywa na Mwalimu Julius Nyerere na 
sasa chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan diplomasia imepaishwa zaidi, 
amefungua nchi, dunia yote inaangalia Tanzania.
“Ujumbe wangu kwa
 vijana kwanza mjiamini na mjue inawezekana, jenga mahusiano , ipende 
kazi unayofanya na muhimu jiheshimu , jiongoze. Kuhusu miaka miwili ya 
Rais Samia hasa katika nyanja ya Diplomasia kuna mengi ya kusherehekea 
pengine inahitaji kupindi maalumu.
“Rais amefungua nchi ambayo 
imetuletea neema , imetuletea faraja katika maeneo yote, diplomasia 
imepaa , amepanga safu nzuri ya diplomasia kutoka nyanja mbalimbali 
maana zamani ilikuwa mwana diplomasia lazima atoke Wizara ya Mambo ya 
Nje lakini yeye amechanganya uzoefu mbalimbali na Tanzania inafika.
“Tunamshukuru
 sana Rais wetu na leo kwenye jumuiko nilikuwa nawaambia mtu usijifanye 
sijui nani , kuwa wewe, mnavyomoona Mama Samia ni Mama Samia, 
tunampenda, tumheshimu, kwa hiyo katika miaka miwili yako mengi na mimi 
nilipata bahati ya kuhudumu nafasi ya Waziri wa Mambo ya Nje kwa zaidi 
ya mwaka mmoja  na nusu na tarehe 19 anapotimiza miama miwili ya uongozi
 wake tutakutana pamoja kwa ajili ya kumpongeza.
Kwa upande wake 
Balozi wa heshima wa Seychell Maryvyonne Poll ambaye amekuwepo nchini 
Tanzania kwa mwaka wa 41 sasa amesema Rais Samia amekuwa mstari wa mbele
 kwenye eneo la diplomasia na tangu ameanza kazi ametumia diplomasia 
katika kutekeleza masuala mbalimbali.
“Diplomasia sio tu lazima 
kuwa balozi bali wanawake wote ni mabalozi kuanzia nyumbani, katika 
biashara na ukweli kwa sasa wanawake tunamfuata Mama samia kwasababu 
yeye ni Mwanadiplomasia namba moja kwa hapa nchini Tanzania,”amesema 
Balozi Pool.
Kuhusu kongamano lililoandaliwa na Taasisi ya 
Wanawake na Diplomasia amesema amefurahi kwani amekutana na wasichana 
wengi na vijana wa Shule ya diplomasia Kurasini, ujumbe wake amewaomba 
kutokana tamaa ili kufanikisha ndoto yao ya kuwa wana diplomasia na wala
 wasiogope.
Wakati huo huo Mkurugenzi na  Mwanzilishi wa Taasisi 
ya Wanawake na Diplomasia Kaneni Mushi amesema tukio hilo 
limewakutanisha mabalozi, wanawake wa taasisi mbalimbali pamoja na 
vijana wanaosomea diplomasia.Lengo kuu ni kumsherehekea mwanamke katika 
sekta nzima ya diplomasia lakini kuunga mkono jitihada za Rais Dk.Samia 
Suluhu Hassan ambaye ndiyo mwanadiplomasia namba moja nchini kwa namna 
anavyopeperusha bendera anavyofungua uchumi na kulifanya taifa kujulina 
duniani.
Ametumia nafasi hiyo kueleza taasisi hiyo imejikita 
katika uchumi wa diplomasia , hivyo wanashukuru wadau wengi kujitokeza 
huku akieleza kufunguliwa kwa milango ya diplomasia nchini wanashuhudia 
maendeleo yanavyoongezeka.
“Tanzania tunatambulika,tunaheshimika
 , tunaona vijana wengi wanafanya vitu vikubwa, wana kampuni zao, wana 
taasisi zao, hivyo tunamshukuru Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa jinsi 
ambavyo amefungua diplomasia ya uchumi.”
Matukio
 mbalimbali katika picha wakati wa Kongamano la Diplomasia 
lililoandaliwa na Taasisi ya Wanawake na Diplomasia kwa ya kujadiliana 
masuala ya diplomasia ikiwemo ya uchumi



.jpeg)

.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...