Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
MKUU wa mkoa wa Pwani, alhaj Abubakar Kunenge amezindua Soko la Utete,lenye vizimba 89 ,ambapo limegharimu kiasi cha sh. milioni 172 .
Akisalimia Wananchi wa Utete wakati wa Uzinduzi huo ,Kunenge ameitaka Halmashauri ya Utete kusimamia upangaji wa wafanyabiashara kwenye Soko hilo ili kuondokana na madalali na kuwa sehemu ya Huduma.
Ameeleza ,Rais Samia Suluhu Hassan, anafanya kazi kubwa kwa Wananchi wa Rufiji ikiwemo Ujenzi wa Miundombinu mbalimbali ili kuwanufaisha wananchi.
Mkuu huyo wa mkoa,amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Rufiji kuanza kupanga Mji wa Utete kwani ni Mji mzuri unaokuwa kwa kasi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...