Na Mwandishi Maalumu -Nigeria

UBALOZI  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Voice of Nigeria, umefungua Darasa la Kiswahili kwa wafanyakazi wa Voice of Nigeria.

Imeelezwa kwamba mafunzo hayo ni kwa ngazi ya awali kwa ajili VON kujiandaa kuimarisha Idhaa yao ya Kiswahili, yalifanyika Mei 9, 2023

Mafunzo yamefunguliwa na Balozi Benson Alfred Bana ambaye ni  Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Nigeria na Mkurugenzi wa VON,  Osita Okechukwu

Aidha, VON September 23, 2022  walisaini hati ya makubaliano na  TBC, ambapo pamoja na mambo mengine kwa ajili ya kushirikiana katika Kutangaza Kiswahili.

Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Dk.Benson Bana akizungumza wakati wa ufunguzi wa darasa la Kiswahili kwa wafanyakazi wa Voice of Nigeria. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...