Na Mwandishi Wetu, DODOMA

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Mhe.Patrobas Katambi amesema serikali inalipa pensheni kwa wastaafu kwa wakati kila ifikapo tarehe 25 ya mwezi.

Mhe.Katambi ameyasema hayo bungeni Mei 26, 2023 alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbogwe (CCM), Mhe. Nicodemus Maganga ambaye ametaka kujua serikali ina mpango gani wa kuhakikisha pesheni za wastaafu zinalipwa kwa wakati.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Katambi amesema katika kuhakikisha wastaafu wanalipwa pensheni zao kwa wakati, Serikali kupitia mifuko ya pensheni ya PSSSF na NSSF imeweka utaratibu mahsusi wa kufanya malipo kwa njia ya kielektroniki kupitia kwenye akaunti zao za Benki kabla au ifikapo tarehe 25 ya kila mwezi.

Aidha, amesema hadi kufikia mwezi Machi 2023 idadi ya wastaafu wanaolipwa pensheni katika Mifuko ya PSSSF na NSSF imefikia 186,605 (ikijumuisha PSSSF wastaafu 158,735 na NSSF wastaafu 27,870).

Naibu Waziri Katambi amesema mifuko inaendelea kuimarisha mifumo ya ndani ya ulipaji wa mafao ili kuhakikisha maombi ya wastaafu wapya yanafanyiwa kazi kwa haraka na kuanza kulipwa pensheni ndani ya kipindi kisichozidi siku 60 kama Sheria inavyotaka.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...