Na.Vero Ignatus,Arusha

Mei 21,2023 Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) wametangaza rasmi  wamefungua dirisha la udahili kwa wanafunzi wanaotaka kujinga na vyuo mbali mbali hapa nchini katika mwaka wa masomo 2023/2024.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Arusha Mkurugenzi wa udhibiti, ufuatiliaji na Tathimini NACTVET Dkt, Jofrey Oleke, amebainisha  kwamba udahili huo wa kozi zote zinazotolewa na vyuo mbali mbali wamefungua rasmi  hadi Juni 30, 2023 katika awamu ya kwanza.

Amesema kuwa wahitimu wote wa Elimu ya Sekondari na vyuo vyenye sifa za kujiunga na kozi za Astashahada na Stashahada, wanashauriwa kufanya maombi yao kwa umakini ili kupata nafasi ya kujiunga na kozi wanazo zipenda". Amesema Dkt Oleke.
 

Amesisistiza kuwa wanafunzi  wote wawe wametimiza sifa na vigezo vya  kujiunga na vyuo katika kozi walizo omba kwa mwaka wa masomo 2023/2024 na maombi hayo ya kujiunga yatumwe katika vyuo husika". Ameongeza Dkt, Oleke.

Sambamba na hayo  Dkt, Oleke alielezea kuwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na programu/ kozi za Afya na Sayansi Shirikishi kwa upande wa Tanzania Bara wanapaswa kuwasilisha maombi yao kupitia udahili wa pamoja .

Dkt, Oleke.wametoa mawasiliano kwa wanafunzi wanaopenda kujiunga na kupitia kozi ya Afya  na Sayansi Shirikishi hawa wanapaswa kuwasilisha maombi yao kupitia udahili wa pamoja yaani Central Admission System _ CAS, katika tovuti ya Baraza  www.nacte.go.tz". Amesema

Mkurugenzi wa udhibiti, ufuatiliaji na Tathimini NACTVET Dkt, Jofrey Oleke, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kufunguliwa kwa dirisha la udahili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...