Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa H. Aweso (Mb) ametengua uteuzi wa Meneja wa Maji Mkoa wa Dodoma, (RUWASA) Mhandisi Godfrey Kabula Mbabaye kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Waziri Aweso amechukua hatua hiyo kwa Mamlaka aliyonayo kupitia Sheria Na. 5 ya Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2019,
Aidha, Waziri Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Nadhifa Kemikimba kuunda timu ya Wataalam ya kufuatilia changamoto ya utekelezaji wa Miradi ya Maji kwa Mkoani Dodoma na kutoa suluhisho la kumaliza changamoto hizo mara moja.
Vilevile, ameelekeza timu hiyo ya Wataalam itakayoundwa na katibu Mkuu ifanye tathimini ya utendaji kazi wa Mameneja wa Wilaya zote wa Maji Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Dodoma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...