Kampuni ya Sukari Kilombero kupitia bidhaa yake ya Bwana Sukari inatumia fursa ya maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam kuonyesha bidhaa zake na kutoa elimu kwa Watanzania kuhusu fursa zilizopo kutokana na uwekezaji unaofanywa na kampuni katika mradi wake wa Upanuzi.

Kwa mara ya kwanza katika maonesho hayo, wateja wanaweza kujionea sukari zilizo katika paketi ndogo za gramu 50, maarufu kama 'Kitamtam' ambazo zinapatikana kwa bei ya reja reja ya shilingi 200/-.

Mbali na 'Kitamtam', kampuni inatoa punguzo la bei katika bidhaa zote kwa wateja wanakaofika katika banda hilo. Pia kuna michezo mbalimbali ambapo wateja wanaweza kujishindia zawadi kutoka kwa Bwana Sukari.

Baadhi ya wateja waliofika katika banda la Kampuni ya Sukari Kilombero kujionea bidhaa mbalimbali za Bwana Sukari.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Sukari Kilombero, Olympia Fraten (kushoto) akijadiliana jambo na Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Kampuni hiyo, Fimbo Butallah katika maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam
Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Kampuni ya Sukari Kilombero, Bw. Fimbo Butallah (mwenye shati nyeupe) kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni hiyo
Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Kampuni ya Sukari Kilombero, Fimbo Butallah (kushoto) katika mazungumzo na Meneja wa Mawasiliano na Mahusiano wa Kampuni hiyo, Willa Haonga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...