VIONGOZI wa Shirikisho la Waendesha Bodaboda Tanzania, leo Agosti 9, 2023 wamefika katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam na kuzungumza na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Ndg. Sophia Mjema.

Viongozi hao walimuomba Ndg. Mjema kumfikishia salamu za pongezi Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoongoza nchi na kutatua kero zinazowakabili wananchi wa makundi mbalimbali wakiwemo wao.

Walimtuma Ndg. Mjema amweleze Rais Dkt. Samia kwamba wanamuunga mkono katika kazi anazofanya kuhakikisha nchi inapata maendeleo na maisha ya Watanzania yanakuwa bora.

Kwa upande wake Ndg. Mjema aliahidi kuzifikisha salamu hizo na kuwashukuru kwa kuendelea kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi.













Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...