Na. Dennis Gondwe, CHANG’OMBE

HALI ya ulinzi na usalama katika Mtaa wa Mazengo ni shwari na wananchi wanaendelea kutekeleza shughuli za maendeleo.

Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Mazengo, Godfrey Nkinda alipowasilosha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Mazengo.

Nkinda alisema kuwa hali ya ulinzi na usalama katika Mtaa wa Mazengo uliyopo Kata ya Chang’ombe ni shwari. “Uongozi wa serikali ya Mtaa wa Mazengo umekuwa ukishirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha mtaa unakuwa salama. Polisi wamekuwa wakikabiliana na matukio madogomadogo ambayo ni viashiria vya uhalifu. Jeshi la Polisi kupitia Polisi kata na jamii wamekuwa wakifanya doria na misako ili kubaini maeneo chochezi ambayo ni vijiwe vya kuvutia bangi hasa maeneo ya Mapagale jambo ambalo Polisi wamefanikiwa kulipunguza na kazi ya kukabiliana na hali hiyo bado inaendelea” alisema Nkinda.

Alisema kuwa vikao vya ulinzi na usalama vimekuwa vikifanyika kupitia Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mtaa kwa kushirikiana na wenyeviti wa mashina ili kuendelea kupeana taarifa juu ya uwepo wa viashiria vya uhalifu.

Kwa upande wake mwananchi wa mtaa huo John Vene alisema kuwa suala la ulinzi na usalama nilawahusu wananchi moja kwa moja. “Hatuwezi kuwategemea Polisi kwa sababu wapo wachache pamoja na kuwa na mafunzo ya kukabiliana na uhalifu” alisema Vene.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...