Na Shamimu Nyaki
WAZIRIwa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amefungua Kikao cha Faragha cha Viongozi wa Wizara na Wakuu wa Taasisi leo Agosti 16, 2023 mkoani Morogoro.

Mhe. Chana amesisitiza kuwa, vikao vya aina hiyo, vinatoa fursa ya kujitafakari kukumbushana namna ya kutekeleza majukumu ya Wizara na Taasisi ili kusaidia mabadiliko zaidi katika nchi.

"Natambua kuwa majukumu ya wizara kwa mujibu wa muundo ni kuhudumia wadau wa sekta tunazozisimamia ili kuhakikisha kuwa matarajio ya Serikali ya Awamu ya Sita pamoja na ya wadau wetu yanafikiwa kwa kiwango kikubwa," amesema Mhe. Chana.

Awali Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Hamis Mwinjuma amesema wizara hiyo inamgusa kila mtu katika kupata burudani, ajira, uhusiano na kipato, ambapo amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye ligi bora Duniani, Wanamuziki wengi wanaounganishwa na lugha ya Kiswahili na kwa sasa inakamilisha maboresho katika Sera ya Utamaduni ili iendane na wakati wa sasa,

Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Malima amesitiza muendelezo wa kuutangaza Utamaduni wa Taifa ili ujulikane kwa mila, desturi na utu wetu bila kusahau sekta yetu ya michezo ambayo inaendelea kukua siku hadi siku.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Saidi Yakubu amesema
Mkutano huo ni Utekekezaji wa maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa mwezi Machi, 2023 jijini Arusha wakati wa kikao cha faragha cha viongozi, na kitakua na mada mbalimbali ikiwemo Vipaumbele na Utekelezaji wa Bajeti ya mwaka 2023/24, pamoja na Mabadiliko ya Taasisi.

Kikao hicho kitafanyika kwa siku tatu kuanzia Agosti 16 hadi 18, 2023 ambacho kinahudhuriwa na Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo, Wakuu wa Taasisi na Wakurugenzi Wasaidizi wa Wizara hiyo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...