Na Asya Khamis  Maelezo  24/8/2023

 

Waziri wa Habari Vijana, Utamaduni,na Michezo Mhe Tabia Maulid Mwita  amewataka wanajamii kuunga mkono na kushiriki kikamilifu  katika uzinduzi wa tamasha la Kizimkazi festival ili kuchochea  maendeleo na ustawi katika jamii.

 

Hayo yameelezwa na Waziri huyo wakati akizungumza na waandishi wa habari huko ofisini Migombani Mjini Zanzibar.

 

Amesema tamasha linatarajiwa kuzinduliwa tarehe 26 mwezi  huu na Raisi wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe D.k Hussein Ali Mwinyi huko Paje Mkoa wa Kusini Unguja.

 

Sambamba  na hayo ameeleza kuwa  shughuli mbalimbali zinaendelea kufanyika ikiwemo kuhamasisha watu kwenye masuala ya michezo, sanaa, na shughuli za kijamii kwa lengo la kuleta maendeleo kwa jamii husika.

 

 Aidha amesema  ushiriki wa  wananchi  utasaidia kujionea mafanikio  ya tamasha hilo pamoja na umuhimu mkubwa katika  kuchochea miradi ya maendeleo. 

 

Waziri tabia aliwashukuru wafadhili mbalimbali waliofanikisha kuunga mkono Tamasha hilo ikiwemo Zanzibar maisha bora foundation, mwanamke initiative foundation pamoja  na Wizara yake inayotoa habari kwa ajili ya kuihabarisha jamii juu ya tamasha hilo

 

Tamasha linatarajiwa kufungwa rasmi tarehe  31 mwezi  huu na Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan  katika maeneo ya Kizimkazi.

 

 

 Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Tabia Maulid Mwita akifafanua jambo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali kuhusiana na Tamasha kubwa la Kizimkazi linalotarajiwa kuanza Kesho 25 Agost,hafla iliofanyika Ofisini kwake Migombani Zanzibar.

 


Waziri wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo Tabia Maulid Mwita akizungumza na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali kuhusiana na Tamasha kubwa la Kizimkazi linalotarajiwa kuanza Kesho 25 Agost,hafla iliofanyika Ofisini kwake Migombani Zanzibar.

 

PICHA  NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR,24/08/2023.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...