KITUO cha Demokrasia Tanzania (TCD) kimefanya kikao na viongozi wa Jumuiya za wanawake wa vyama wanachama wa TCD kujadili namna ya kuanzisha jukwaa la wanawake chini ya Kituo hicho.

Kikao hicho kimefanyika katika ofisi za Kituo cha Demokrasia Tanzania zilizopo Mikocheni jijini Dar es Salaam leo Agosti 09, 2023 huku vyama; CHADEMA, CCM, CUF, ACT-WAZALENDO pamoja na NCCR - Mageuzi wakishiriki.

CHAUMMA wameshiriki kuwakilisha vyama visivyo na wabunge/madiwani.

Jukwaa hilo linaundwa ili kuwakutanisha pamoja viongozi wa Jumuiya za wanawake za vyama wanachama wa TCD kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kutatua changamoto za wanawake katika siasa na uongozi.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...