Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV
MENEJA wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa kikodi Kinondoni mkoani Dar es Salaam Husna Nyange amesema kodi sahihi inatokana na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo amewahimiza wafanyabiashara kutoa risiti kila wanapofanya mauzo.
Pia na wanunuzi kudai risiti sahihi za EFD kila wanaponunua bidhaa au kupata huduma lengo likiwa kila mmoja kwa nafasi yake anatunza kumbukumbu zake.
Nyange ameyasema hayo leo Agosti 24, 2023 wakati wa uzinduzi wa uzinduzi wa mabango ya uhamasishaji kuhusu matumizi sahihi ya EFD
Hivyo pamoja na mambo mengine ameelezea umuhimu wa wafanyabiashara kuwa na kumbukumbu sahihi za kikodi hivyo lakini wanunuzi nao ni vema wakajenga utamaduni wa kudai risiti kutoka kwa wafanyabiashara.
Kwa upande wake Meneja Msaidizi wa Huduma kwa Mlipakodi Mkoa wa kikodi Kinondoni Emanuel Lucian Dafay amesema kampeni hiyo ya EFD ni endelevu na kwa mkoa wa Kinondoni walianza kwa kutuma ujumbe mfupi (sms) kwa wafanyabiashara kupitia simu zao za mkoni.
Amefafanu lengo la kutuma ujumbe ili kuwakumbusha kuhusu wajibu wao wa kutoa risiti sahihi za EFD.“Wafanyabiashara wa Mkoa wetu wa Kinondoni wamepata meseji za kuwakumbusha umuhimu wa kutoa risiti, "amesema.
Wakati huo huo wafanyabiashara wameipongeza TRA kwa kuendelea kuwakumbusha wajibu wao kuhusu mambo mbalimbali ya kikodi ikiwemo kutoa na kudai risiti.
Pia wafanyabiashara wamehaidi kutimiza wajibu wao wa kutoa risiti kila watakapofanya mauzo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...