Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Namibia, Bi. Upendo Mwasha (kushoto) akimwonesha mteja vazi aina ya batiki kutoka Tanzania wakati wa Maonesho ya Mwaka ya Kibiashara ya Ongwediva ambayo yanafanyika nchini humo kuanzia tarehe 27 Agosti, 2023. Maonesho hayo ambayo yalifunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara wa Namibia, Mhe. Verna Sinimbo yamewashirikisha Wajasiriamali kutoka Tanzania na Diaspora wanaoishi nchini Namibia. Mbali na kuonesha bidhaa mbalimbali za Tanzania, Ubalozi umetumia maonesho hayo kutangaza Lugha ya Kiswahili kwa kuweka vitabu vya kiswahili katika Banda la Ubalozi na kuhamasisha wateja kusoma na kujifunza Lugha hiyo kupitia Ubalozi ambao umeanzisha Maktaba ya Kiswahili.


Wadau mbalimbali wakitembelea Banda la Tanzania kwenye maonesho hayo

Baadhi ya Wajasiriamali wa Tanzania wakishiriki maonesho ya Mwaka ya Kibiashara ya Ongwediva yanayofayika nchini Namibia

Banda la Tanzania kama linavyoonekana pichani. Bidhaa mbalimbali kutoka Tanzania zinazooneshwa kwenye maonesho hayo ikiwa ni pamoja na nguo za batiki, vikapu, viatu vya asili, shanga, kahawa na majani ya chai.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...