Na Rahma Khamis Maelezo.                     24/8/2023.

 

Maafisa na Wapiganaji wa Chuo Cha Mafunzo Zanzibar wameuomba Mfuko wa huduma za Afya (ZHSF) kuharakisha malipo katika vituo vitakasvyochaguliwa kutoa huduma ili kuondosha usumbufu unaoweza kujitokeza.

 

Wakitoa maoni katika kiao cha kuhamasisha kujiunga na Mfuko huo katika chuo cha Mafunzo magereza wamesma kuchelewa kuwasilisha  fedha katika vituo hivyo kwa wakati  kutazorotesha utoaji wa huduma bora vituoni humo.

 

Aidha walifahamisha kuwa fedha hizo zinazotoka katika mfuko huo ndizo wanazotumia kupata mahitaji ya huduma za afya kwa wananchi ikiwemo vifaa tiba.

 

“ikiwa tutakaa kwa muda mrefu hatujaletewa fedha ambazo zitasaidia kununulia vifaa kama madawa na vifaa vyengine wananchi wetu watashindwa kufika katika hospitali zetu na kwenda kutafuta huduma vituo vyengine,”walifafanua  maafisa hao.

 

Mapema  Kaimu Mkurugezi Mkuu wa Mfuko huo  Yassir Ameir Juma amewataka wananchi kuondoa  hofu  kwani Mfuko huo unatarajia kuufanya kila jitihada kuhakikisha  hakutakua na malalamiko  katika vituo vyote  juu ya utoaji wa huduma hiyo.

 

Amesema mfuko huo utakapoanza kutoa huduma hizo kututakua na utaratibu maalumutakaotumika kwa wagonjwa ili kupunguza gharama za matumizi katika mfuko huo.

                                                                                           

Amefahamisha kuwa mfuko  hautoishia zanzibar kama baadhi ya watu wanavyosema  kwani wanaandaa mikakati madhubuti kwakushirikiana na Mfuko wa Bima  ya Afya wa Tanzania kuhakikisha wananchi wote wanapata  huduma  katika  maeneo yao.

 

Aidha amesema huduma zote za msingi zitakuwepo katika mfuko huo ili kuepusha usumbufu kwa  wagonjwa ambao wanahitaji matibabu.


Akifafanua zaidi  Kaimu amesema matibabu ni msingi wa maisha ya binadamu hivyo mfuko utafanya kila jitihada kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora na zauhakika bila ya usumbufu.

 

Aidha amefahamisha kuwa mwananchi endapo ataumwa lazima anzie Kituo cha afya kilicho karibu na endapo  atapata rufaa ndipo ataendelea kwenda hospitali nyengine kwa ajili ya  matibabu zaidi.  

 

"Kama hatutaweka utaratibu maalumu  gharama itakuwa kubwa na ili mfuko uendelee kuwepo lazima utaratibu huo utumiwe kwani unahitaji kulindwa ili ubaki salama" alieleza.

 

Hata hivyo Kaimu amewataka watoa huduma kuwa na kauli nzuri kwa wagonjwa ili kuepusha malalamiko kwa baadhi ya wagonjwa .

 

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mfuko wa huduma za Afya  Zanzibar Yassir Ameir Juma  akizungumza  na maafisa na wapiganaji wa Chuo cha Mafunzo wakati akihamasishaji maafisa hao  kujiunga na  mfuko huo ,huko Makao Makuu ya Chuo hicho  Kilimani Mjini Unguja .

 Kamishna wa Chuo cha Mafunzo Khamis Bakari Khamis akizungumza wakati akaimkaribisha Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mfuko huduma za Afya  Afya  Zanzibar Yassir Ameir Juma  kuzungumza na maafisa na wapiganaji wa Chuo hicho juu ya dhana ya mfuko huo, huko Makao Mkuu ya Chuo hicho Kilimani Mjini Unguja.

Naibu Kamishna Chuo cha Mafunzo Hamdu Haji akiuliza swali kwa watendaji wa mfuko wa huduma za Afya  walipofika kuhamasisha maafisa wa Chuo hicho kujiunga na  mfuko huo huko Makao Makuu ya Chuo hicho  Kilimani Mjini Unguja

Afisa wa Chuo cha Mafunzo Sada Nassor akiuliza suali kwa watendaji wa mfuko wa huduma za Afya  walipofika kuhamasisha maafisa wa Chuo hicho kujiunga na  mfuko huo, huko Makao Makuu ya Chuo hicho  Kilimani Mjini Unguja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...