Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga wametembelea Bandari zinazosimamiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa ajili ya kujionea na kujifunza namna zinavyofanya kazi. 

Bandari walizotembelea ni pamoja na Bandari ya Nchi Kavu ya Isaka wilayani Kahama Mkoa wa Shinyanga pamoja na Bandari za Ziwa Victoria (Kusini na Kaskazini)


Wakitembelea bandari hizo Agosti 30,2023,  waandishi wa habari wamejionea namna Serikali inavyowekeza kwa kufanya maboresho makubwa kwenye Bandari hizo na kuchochea ukuaji wa uchumi hapa nchini.

Meneja Bandari za Ziwa Victoria Frednand Nyathi, amesema katika maboresho ya Bandari tatu za Mwanza Kaskazini, Kemondo na Bukoba, Serikali imetenga kiasi cha fedha Sh. bilioni 60 kwa ajili ya kuzikarabati.

Amesema maboresho hayo yataongeza ufanisi wa utendaji kazi wa Bandari pamoja na kuongeza mapato na kukuza uchumi wa nchi.

Afisa Bandari ya Isaka wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Abel Mshana amesema Bandari hiyo imekuwa ikiwahudumia wateja wa ndani na nje ya nchi na imekuwa ikirahisisha utendaji wa bandari na imekuwa ikihudumia nchi tano kusafirisha mizigo ikiwemo Rwanda,Burundi,Uganda, Sudani Kusini na DRC.

 Amewashauri wafanyabiashara na wadau kutumia bandari hiyo ili kupunguza gharama na muda wa kusafirisha mizigo.

Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga (SPC) iliyoandaa ziara hiyo, Greyson Kakuru amesema katika ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ya uwekezaji wa Bandari ambao ni kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi hapa nchini ikiwemo maboresho makubwa ya bandari.

Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria

Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Meneja wa Bandari za Ziwa Victoria Ferdinand Nyathi akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria

Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi Mkoa wa Shinyanga, Greyson Kakuru akizungumza wakati waandidhi wa habari walipotembelea Bandari za Ziwa Victoria
Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria
Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria
Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria
Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria

Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria



Waandishi wa habari wakitembelea Bandari za Ziwa Victoria
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Waandishi wa habari wakitembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Waandishi wa habari wakitembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Afisa Bandari ya Nchi Kavu Isaka mkoa wa Shinyanga Abel Mshang'a akizungumza na waandishi wa habari walipotembelea bandari ya Nchi Kavu Isaka
Waandishi wa habari wakipiga picha ya kumbukumbu katika bandari ya Nchi Kavu Isaka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...