Agosti 22, 2023 Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amekutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mkazi Mpya “Mission Director” wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID), Craig Hart ofisini kwake jijini Dodoma.

Mazungumzo hayo yalilenga zaidi mashirikiano katika kuboresha matumizi ya Teknolojia ili kuwezesha huduma nyingine zikiwemo Kilimo na Afya, mashirikiano katika kukuza Taasisi changa za Startup, mashirikiano katika kuwezesha miji ya kisasa (Smart City) pamoja na kutumia Teknolojia mpya ya 5G katika kuboresha uchumi wa Kidijitali.

Pia ziara hiyo ya Craig Hart ilikuwa ni kujitambusha kama Mkurugenzi Mkazi mpya wa Shirika la Kimarekani la USAID nchini Tanzania huku akichukua nafasi ya Bi. Kate Somvongsiri aliyemaliza muda wake.

#TzyaKidijitali #KaziIendelee




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...