NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na alama tatu kwa kuweza kuinyuka KMC FC 5-0, kwenye mchezo wa ligi Kuu NBC uliopigwa kwenye dimba la Azam Complex Jijini Dar es Salaam.

Katika Mchezo huo Yanga iliwaanzisha baadhi ya nyota wao akiwemo Pacome Zouzoua ambaye amekuwa nyota wa mchezo kwa kufanikiwa kufunga bao moja na kutengeneza lingine kuisaidia timu yake kuondoka na ushindi mnono.

Zouzoua ameonesha uwezo wake na kuvuta hisia za mashabiki ambao walifika uwanjani wakishangilia pindi anapogusa mpira  na kupeleka mashambulizi kwa wapinzani.

Dickson Job alianza kuandika bao la kwanza kipindi cha kwanza mara baada ya kupiga shuti la kisigino kipa wa KMC na kuokoa hivyo Job akapata nafasi tena ya kufunga bao ambalo lilidumu mpaka mapumziko.

Mabao mengine ya Yanga Sc yamewekwa kimyani na Mudathir Yahya, Aziz Ki pamoja na KonKoni.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...