Na John Walter-Manyara

Mbunge wa jimbo la Babati mjini na naibu waziri wa katiba na sheria Mhe. Pauline Gekul leo amekutana na Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Maji na Nishati [Ewura CCC] Mkoa wa Manyara na kuitaka taasisi hiyo kushiriki katika mikutano ya wananchi kwa lengo la kutatua na kusikiliza kero za wananchi.

Mhe. Gekul ametoa wito huo ili kuongeza juhudi za kutoa elimu na kusikiliza kero za wananchi wanazopata kuhusiana na  huduma za maji,Nishati ya Umeme na Gesi kupitia mikutano ya hadhara ili wananchi waitambue taasisi hiyo

Kwa upande wake Afisa Msaidizi Huduma kwa wateja na utawala kutoka 
Ewura CCC -Manyara bi Neema Nnko amesema lengo la kukutana na mbunge huyo ni kuitambulisha taasisi hiyo na kushirikiana na mbunge huyo ili kutatua kero za wananchi.

Aidha ameongeza Kuwa [EWURA CCC] ipo kwaajili ya kuwatetea watumiaji wa huduma za maji, umeme na gesi kama iwapo wamekutana na changamoto zozote na kutoridhishwa na huduma hizo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...