Na John Walter-Manyara
Mbunge wa jimbo la Babati mjini na naibu waziri wa katiba na sheria Mhe. Pauline Gekul leo amekutana na Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Maji na Nishati [Ewura CCC] Mkoa wa Manyara na kuitaka taasisi hiyo kushiriki katika mikutano ya wananchi kwa lengo la kutatua na kusikiliza kero za wananchi.
Mhe. Gekul ametoa wito huo ili kuongeza juhudi za kutoa elimu na kusikiliza kero za wananchi wanazopata kuhusiana na huduma za maji,Nishati ya Umeme na Gesi kupitia mikutano ya hadhara ili wananchi waitambue taasisi hiyo
Kwa upande wake Afisa Msaidizi Huduma kwa wateja na utawala kutoka
Ewura CCC -Manyara bi Neema Nnko amesema lengo la kukutana na mbunge huyo ni kuitambulisha taasisi hiyo na kushirikiana na mbunge huyo ili kutatua kero za wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...