Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Ndugu Elias M. Kayandabila amemtaka Mkuu wa Kitengo cha Taka Ngumu Ndugu Adamu Baleche kuhakikisha kuwa ndani ya siku tatu awe ameondosha taka zote zilizopo maeneo yote ya kukusanyia taka na kuzipeleka dampo. 

Kanyandabila ameyatoa maelekezo hayo leo Septemba 18, 2023 wakati wa Ziara fupi ya Timu ya Menejimenti ya Halmashauri (CMT) ya kukagua hali ya usafi katika viunga vya Manispaa ya Tabora.

Aidha Ndugu Kayandabila ameunda timu ndogo itakayoshirikiana na Kitengo cha Taka Ngumu katika kuratibu na kusimamia kazi zote za usafi mjini hapo, lengo kubwa ikiwa ni kuongeza ufanisi wa shughuli za usafi katika Manispaa yetu.

Wajumbe wa CMT nao baada ya kujionea hali mbaya katika maeneo ya kukusanyia taka, wameafiki kwa pamoja umuhimu wa timu hiyo ndogo ambayo itaongeza nguvu kwenye kitengo cha taka ngumu.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...