Na WHMTH, Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. John Mongella amewakaribisha wananchi wa jiji la Arusha kushiriki uzinduzi wa jengo la Ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) lililopo barabara ya Moshi, mtaa wa Sekei jirani na hoteli ya Mount Meru.
Mhe. Mongela ametoa mwaliko huoleo Septemba mosi, 2023 jijini Arusha ambapo ametoa ya Mgeni rasmi atakayezindua jingo hilo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mnamo tarehe 2 Septemba, 2023.
Ameongeza kuwa ufunguzi wa jengo hilo ambalo Tanzania imeshiriki kulijenga ni uthibitisho tosha wa jitihada za Serikali iliyopo madarakani katika kujipambanua na kuleta mageuzi makubwa katika sekta zote ikiwepo sekta ya habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.
Katika hatua nyingine, Mhe. Mongella amewataka wananchi wa Arusha kuendelea kuwa wakarimu na kuwakaribisha wageni wetu, wakiwemo Mawaziri kutoka nchi wanachama wa PAPU, Mkurugenzi Mkuu wa Umoja wa Posta Duniani (UPU) Bw. Mesahiko Metoki pamoja wajumbe kutoka nchi wanachama wa PAPU.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...