Na Nasra Ismail, Geita

Akizungumza na watumishi wa serikali katika halmashauri ya mji wa Geita Waziri wa nchi Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala bora George Simbachawene alisema kuwa waliofanya udanganyifu tayari wameshajulikana na wanasubiri kuchukuliwa hatua.
Simbachawene aliongeza kuwa watumishi wengi wana uhamisho ambao ni wa uongo na utapeli na pia wameupata kwa kutoa rushwa.
Aidha Simbachawene aliwaasa watumishi ambao wamefanya udanganyifu ili kupata uhamisho warudi walikotoka kwani wasipofanya hivyo watafukuzwa kazi.
“tukigundua tutawarejesha walikotoka, na kwa maneno haya nayosema yule ambaye alihama kwa uhamisho wa uongo uongo na ameshindwa kuhamisha mshahara wake navoongea hapa arudi alikotoka vinginevyo atafukuzwa kazi” alisema Simbachawene.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...