Waziri
wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akiwa katika kikao kazi na
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti kilichofanyika
ofisini kwake jijini Dodoma mapema leo Septemba 26, 2023.
Katika
kikao hicho pamoja na mambo mengine walijadiliana kuhusu dira na
muelekeo wa utekelezaji wa majukumu na shughuli mbalimbali za kila siku
za Wizara katika kuwahudumia wananchi na kutimiza maono ya Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Viongozi wengine walioshiriki katika kikao kazi hicho ni Naibu Katibu Mkuu (Mifugo), Dkt. Daniel Mushi na Naibu Katibu Mkuu (Uvuvi), Bi. Agnes Meena.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...