Na Oscar Assenga, TANGA

JUMUIYA ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga imepongeza Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) huku wakihaidi kuendelea kumuunga mkono na kumuombea kwa Mwenyezi Mungu katika majukumu yake hayo.

Pongezi hizo zilitolewa leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga Hamza Bwanga wakati akizungumza na mtandao huo ambapo alisema kwamba wanaamini kwamba kuchaguliwa kwake kumekuja wakati muafaka kutokana na utendaji wake mahiri katika kuongoza Bunge la Tanzania.

Alisema kuchaguliwa kwake ni kutokana na jitihada zake katika utendaji wake ambao umejengwa na uchapakazi, uzoefu, uaminifu na uadilifu ambao umekuwa ni chachu kubwa kufikia mafanikio hayo.

“Sisi kama Wazazi wilaya ya Tanga tunakupongeza sana Spika wa Bunge kuwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa umoja huo na tunahaidi kumuunga mkono na nafasi hii imekuja wakati muafaka kabisa kwa kuwa yeye ni spika na mchakapazi,mwerevu msikivu “Alisema

Hata hivyo alisema kwamba wao wataendelea kumuunga mkono na kumuombe kwa mwenyezi mungu ili kutenda vema majukumu yake kwa waledi mkubwa .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...