Utiaji saini wa kuanza kwa Mradi wa ujenzi wa miundombinu ya usambazaji Maji Dar es salaam ya Kusini umesainiwa leo kati ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) na Mkandarasi Kampuni ya Sinohydro Corporation Ltd na kushuhudiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Ndugu Kiula Kingu.
Mradi huu utahusisha ujenzi wa tanki kubwa la kuhifadhi maji la lita milioni 9, ujenzi wa kituo cha kusukuma maji na ulazaji wa bomba kwa umbali wa kilomita 25 na unategemea kunufaisha wananchi takribani 450,000 katika majimbo ya uchaguzi ya Kibamba, Segerea, Ukonga, Ubungo,Temeke na Ilala.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...