Na Mwandishi wetu, Babati 
 
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe ameipongeza Kampuni ya Mati Super Brands ambao ni wazalishaji wa vinywaji vikali kwa uwekezaji wa viwanda walioufanya na kushiriki kudhamini maonyesho ya Tanzanite Manyara Trade Fair yanayoendelea katika viwanja vya Stendi ya zamani ya Mjini Babati Mkoani Manyara.
 
Akizungumza mara baada ya kutembelea banda la kampuni ya Mati Super Brands Limited Naibu Waziri Kigahe amepongeza juhudi za kampuni hiyo katika kuwekeza na kulipa kodi stahiki ya Serikali.
 
Kigahe amesema kampuni hiyo imekua mstari wa mbele katika kutoa misaada kwa jamii inayowazunguka pamoja na kudhamini matukio mbali mbali ya kijamii na kiserikali.
 
Hata hivyo, Meneja Masoko wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited Elvis Peter amesema kuwa kampuni hiyo itaendelea kuzalisha bidhaa zenye ubora wa kitaifa na kimataifa.
 
“Kampuni yetu imekua ni wadhamini wakuu wa Maonyesho ya Tanzanite Manyara TRADE FAIR ambayo yanakutanisha wafanyabishara kutoka ndani na nje ya nchi,” Ameeleza Elvis.

Mmoja kati ya wajasiriamali walishiriki maonyesho hayo, Elias Baha amesema wawekezaji wengi zaidi waende kuwekeza kwenye mkoa huo ili jamii ipate ajira kama ilivyofanya kampuni ya Mati Super Brands LTD.

"Wawekezaji wengi zaidi tunawataka mje kuwekeza Manyara mfanye mambo mengi kama ilivyo Mati ni pana ndiyo sababu tunawapongeza kwa uwekezaji wao," amesema Baha.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...