Na.WAF, Dodoma

Naibu Waziri wa Afya leo Tarehe 31, Oktoba, 2023 amekutana na Rais wa Shirika la Kimatifa la Pathfinder Afrika, Bi. Saloucou Zoungrana ambaye amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha kupunguza uwiano wa vifo vya akinamama wajawazito nchini Tanzania.

Bi.Zoungrana ameishukuru Seerikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha uanzishaji Programu ya M-mama EmTS nchi nzima.

Aidha ameahidi kuendelea kujitolea kupitia Shirika la Kimatifa la Pathfinder katika kuendeleza afua za afya hususani Afya ya Uzazi kwa vijana, afya ya mama na mtoto na afya ya watu na mazingira

Naye Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan inaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wa maendeleo ikiwa ni pamoja na Shirika la Kimatifa la Pathfinder

Bi. Zoungrana ameambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Tanzania Shirika la Pathfinder Dkt Joseph Komwihangiro pamoja na Mratibu wa Programu ya M-Mama nchini Tanzania kutoka Shirika la Kimataifa la Pathfinder.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...