
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya Waziri Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imekubaliana kushirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Austria juu ya kufungua fursa za ajira kwa watanzania nchini humo.
Ajira hizo zitawahusisha watanzania wenye ujuzi na ambao hawana na kuwaongezea ujuzi katika sekta ya kilimo, viwanda na biashara.
.jpeg)
Mhe. Katambi amesema wamekubaliana kujifunza namna ambavyo wanaendesha Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na elimu ya ufundi ambapo hadi sasa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivyo nchi nzima.
“Austria wana uzoefu, ujuzi na ubobevu katika masuala ya kiuchumi, ajira na elimu hivyo tunataka kutumia nafasi hiyo kufungua fursa kwa vijana wa kitanzania kujifunza namna ambavyo wenzetu wanafanya” amesema

.jpeg)

.jpeg)

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...