
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akifurahia jambo na Spika wa Seychelles Mhe. Roger Mancienne (katikati) pamoja na Naibu Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Mussa Zungu walipokutana katika Ukumbi mdogo wa Mikutano wa Bunge la Angola uliopo Jijini Luanda nchini Angola leo tarehe 23 Oktoba, 2023. Dkt. Tulia anagombea nafasi ya Urais wa Umoja wa Mabunge duniani (IPU) unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 nchini humo.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson (katikati), akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Namibia Mhe. Peter Katjavivi (kushoto) pamoja na Spika wa Bunge la Zambia Mhe. Nelly Mutti (kulia) wakati walipokutana katika Ofisi ndogo za Bunge la Angola wakati wa Mkutano wa 147 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) ukiendelea nchini humo leo tarehe 23 Oktoba, 2023


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 23 Oktoba, 2023 akizungumza na Wajumbe wa kundi la Latini na Amerika kusini katika ukumbi mdogo wa Bunge la Angola wakati wa Mkutano wa 147 wa IPU akiwaomba wampigie kura katika Uchaguzi wa Urais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) unaotarajiwa kufanyika tarehe 27 Oktoba, 2023 nchini humo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...