NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

KATIKA Kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Kike Duniani, Mtandao wa Jinsia Tanzania imekuwa mstari wa mbela katika kuhakikisha watoa mafunzo jinsi ya kuendelea kumlinda mtoto wa kike dhidi ya ukatili kwenye jamii na maeneo mengine yanayomzunguka.

TGNP imekuwa na Kampeni za mara kwa mara kuhakikisha mwanamke anapata haki zake zote za msingi, na miongoni mwa kampeni ambazo wamkuwa wakizifanya ni pamoja na kampeni ya kupinga ukukutaji kwa watoto wa kike, kampeni ambayo ilibeba kauli mbiu "HAKEKETWI MTU ilikuwa ni kipinndi ambacho mtoto wa kike anapelekwa kwenye Mila za ukeketaji.

Akizungumza leo Oktoba 11,2023 katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS), Mwanaharakati Bi.Zawadi Kondo amesema katika kuhakikisha mwanamke anakomboka kifikra, wameangazia jitihada mbalimbali katika kuendelea kumlinda mtoto wa kike na kumjengea uwezo katika masuala ya Uongozi.

"Tumeona vitu mbalimbali TGNP wamefanya kama kuanzisha vilabu vya jinsia mashuleni ambavyo vimekua chachi katika malezi ya mtoto na vile wanavyo fundishwa na walimu ambao ni walezi wao"Amesema

Aidha Bi. Zawadi ameipongeza TGNP katika jitihada zao katika urekebishwaji au Ushauri wa Sera ambazo zinatengenezwa na Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha jamii inaishi kwa usawa na kupata haki zote za msingi.








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...