Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
BALOZI wa Urusi nchini Tanzania, Andrey Avetisyan amesema ushirikiano uliopo baina ya nchi yao na Tanzania ni mzuri ambapo unasaidia pia kuleta na kukuza maendeleo ya uchumi baina ya mataifa hayo mawili kupitia sekta mbalimbali.

Akizungumza kwenye Kongamano mahsusi lililoandaliwa kuonyesha ‘Robots’ kwa Wanafunzi wa Vyuo mbalimbali wanaosoma masomo ya Sayansi, Mhe. Avetisyan ushirikiano huo utasaidia pia kuleta maendeleo endelevu kupitia matumizi ya teknolojia hizo za kisasa.

“Tunamshukuru sana Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye pia ameonyesha ushirikiano na uhusiano mzuri baina yetu sisi kama mataifa, sisi Urusi tutaendelea kushirikiana na Tanzania katika kila sekta za maendeleo,” amesema Mhe. Avetisyan

Kwa upande wake, Mtaalamu wa Lugha ya Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Prof. Mutembei amewataka vijana wa Tanzania wanaosoma masomo ya Sayansi kutumia fursa hizo za ushirikiano na taifa la Urusi ambayo wanaleta teknolojia hiyo ya ‘robots’

“Kupitia teknolojia hizo zinazoletwa na wenzetu waliopiga hatua kwenye maendeleo, tunawasihi vijana wetu watumie teknolojia hizi kama hawa ‘robots’ kwenye Kilimo kwenye masuala ya Afya,” amesema Prof. Mutembei.

Naye, Shujaa wa Urusi, Mwanaanga mstaafu wa Urusi na Mkongwe aliyekwenda anga za juu mara nne, Anton Shkaplerov amesema teknolojia hizo za ‘robots’ zitasaidia vijana wa Tanzania kuisaidia nchi yao kupiga hatua za maendeleo katika Sekta mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...