Daktari kutoka timu ya Afya Check, Dkt. Elias Joseph (kushoto) akizungumza na mmoja wa wakazi wa Mwanza waliojitokeza kupata ushauri na matibabu ya bure yanayoendeshwa na msafara wa Twende Butiama katika viwanja vya Furahisha jijini humo. Msafara huu ambao umedhaminiwa na asasi ya Vodacom Tanzania Foundation unajumuisha waendesha baiskeli takribani 200 walioanza safari jijini Dar es Salaam Oktoba mosi na wanatarajia kufika Wilayani Butiama Oktoba 14 ikiwa ni juhudi za kuenzi maisha na urithi wa Mwalimu Nyerere kupitia utekelezaji wa shughuli za elimu, mazingira, na afya.
Baadhi ya wakazi wa Mwanza wakipatiwa huduma na madaktari waliokuwepo wakati wa kambi ya matibabu ya bure iliyoendeshwa na msafara wa Twende Butiama katika viwanja vya Furahisha jijini humo. Msafara huu ambao umedhaminiwa na asasi ya Vodacom Tanzania Foundation unajumuisha waendesha baiskeli takribani 200 walioanza safari jijini Dar es Salaam Oktoba mosi na wanatarajia kufika Wilayani Butiama Oktoba 14 ikiwa ni juhudi za kuenzi maisha na urithi wa Mwalimu Nyerere kupitia utekelezaji wa shughuli za elimu, mazingira, na afya.
Baadhi ya wakazi wa Mwanza wakiwa katika foleni kupata huduma wakati wa kambi ya matibabu ya bure iliyoendeshwa na msafara wa Twende Butiama katika viwanja vya Furahisha jijini humo. Msafara huu ambao umedhaminiwa na asasi ya Vodacom Tanzania Foundation unajumuisha waendesha baiskeli takribani 200 walioanza safari jijini Dar es Salaam Oktoba mosi na wanatarajia kufika Wilayani Butiama Oktoba 14 ikiwa ni juhudi za kuenzi maisha na urithi wa Mwalimu Nyerere kupitia utekelezaji wa shughuli za elimu, mazingira, na afya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...