Na: Calvin Gwabara – Nairobi.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda ameongoza timu
ya Serikali ya Tanzania kwenye mkutano mkubwa wa Teknolojia za Kilimo
Afrika (ACAT) ulioanza leo jumatatu nchini Kenya.

Mara baada ya kufika kwenye viwanja vya mkutano huo mkubwa
akiongozana na Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Balozi Dkt. Benard
Yohana Kibesse pamoja na Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Sayansi na
Teknolojia (COSTECH) Dkt. Amos Nungu na watumishi wengine wa
Serikali ametembelea maonesho mbalimbali ya Teknolojia za kilimo
zinazooneshwa nje ya mkutano huo.

“Nimeona maonesho ambayo kimsingi ni kuhusu jinsi Sayansi na
Teknolojia inavyoweza kuleta mabadiliko chanya kwenye kilimo pamoja na
ukweli huu tumeona pia umuhimu wa kuzingatia usalama na afya kwenye
mabadiliko haya na pia kuchukua tahadhari tusipoteze umiliki wa yale
tunayogundua, hasa mbegu bora, ili tusiingie kwenye utegemezi
utakaotudhoofisha” alisema Prof. Mkenda.

Tanzania kupitia wizara yake ya Elimu Sayansi na Teknolojia na taasisi
zilizo chini yake imekuwa ikitoa mchango mkubwa katika kuhakikisha nchi
inawezesha wabunifu kupitia Programu zake mbalimbali ikimwemo.

Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu ( MAKISATU)
ambayo yanafanyika kila mwaka kwa kuhusisha wabunifu mbalimbali
kuanzia kwenye jamii, Shule za Msingi na Sekondari, Vyuo Vya kati, Vikuu
pamoja na Taasisi za Utafiti na kuwapatia washindi fedha na mahitaji
mengine ili kuwezesha kukuza bunifu zao na kuzibiasharisha.

Mkutano huo utazinduliwa siku ya jumanne ya tarehe 31/10/2023 na Rais
wa Jamhuri ya watu wa Kenya Mhe. Dkt. William Samoei Ruto na
kuhudhiriwa na mamia ya wadau wa kilimo kutoka Afrika na Dunia nzima.

Aidha Mkutano huo wa (ACAT) umeandaliwa na Serikali ya Kenya kupitia
Wizara yake ya Kilimo na Maendeleo ya Ufugaji kwa kushirikiana na
Taasisi ya Teknolojia za Kilimo Afrika (AATF)



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...