Na Said Mwishehe, Michuzi TV

ASASI ya AGENDA kwa kushirikiana na Tanzania ConsumerAdvocacy and Research (TCAR) wameitaka Serikali na madaktari wa tiba ya Kinywa na meno kusitisha kutumia dawa yenye zebaki ya kuzoba meno yaliyotoboka kwa makundi yanayoathirika kwa urahisi kama watoto, wanawake wajawazito na wanaonyonesha.

Wamesema hayo wakati wa kuadhimisha Wiki ya Afrika kupinga matumizi ya dawa yenye Zebaki ya kuziba meno yaliyotoboka huku wakieleza kuwa Zebaki imekuwa na madhara makubwa katika afya ya mwanadamu , hivyo ni vema ikasitishwa ili isitumike kama hatua ya kuepusha madhara kwa jamii.

Ofisa Programu Mwandamizi wa AGENDA Dorah Swai amesema katika kuadhimisha wiki hiyo ya kupinga matumizi ya Zebaki katika kuziba meno wameamua kuungana ili kutoa sauti ya pamoja ili Serikali na madaktari wa meno kuacha kutumia Zebaki.

" Wiki ya Afrika ya kupinga matumizi ya dawa yenye zebaki ya kuziba meno yaliyotoboka huwa inaadhimishwa kwenye wiki ya 13 - 20 Oktoba ya kila mwaka lakini kwa mwaka huu tunaiadhimisha kuanzia Novemba 13 mpaka Novemba 18.

"Tumelazimika kufanya hivyo Ili kuruhusu wadau kushiriki katika Mkutano Mkuu wa Tano wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Minamata(the FiRh Conferenceof Partiesof the Minamata Conventionon Mercury(COP5)) pamoja na kupata fursa ya kuzingatia masuala ya mkutano huo.

" Hivyo AGENDA for Environment and Responsible Development (AGENDA) na Tanzania ConsumerAdvocacy and Research (TCAR), pamoja na wadau wengine tumeungana kuadhimisha wiki kama sehemu ya kuunga mkono taasisi nyingine za kiraia zaidi ya 40 barani Afrika katika maadhimisho ya wiki hii muhimu, "amesema Swai.

Aidha amesisitiza lengo kuu la mwaka huu ni kuitaka serikali na nadaktari wa ya Kinywa na Meno (Dentists)wasitishe kutumia dawa yenye zebaki ya kuzİba meno yaliyotoboka(kwa Kiingereza DentalAmalgam) kwa makundi yanayoathİrika kwa urahisi.

Ameongeza kwamba wanatarajia iwe hivyo pia kwa makundi mengine siku zijazo huku akifafanua huu ni mwaka wa 10 tangu waanze kushiriki maadhimisho hayo kuanzia yalipozinduliwa mwaka 2014.

Aidha amesema mwito huo unaendana na matakwa ya Mkataba wa Minamata uliopitishwa mwaka 2013 na nchi zipatazo 140 ikiwemo Tanzania, mara tu baada ya kupitishwa, na Tanzania ikauridhia Oktoba 5, 2020.

Ameongeza kuwa katika mkataba huo kuna marekebisho kadhaa yamefanyika likiwemo rekebisho la watoto linalozitaka nchi wanachama kutotumia‘ Dental Amalgam’ kwa kuzibia meno ya watoto na wanawake wajawazito na wanaonyonyesha.

"Dental Amalgami na zebaki kwa asilimia hamsini, inadhuru wanadamu na mazingira.Kama sehemu ya utekelezaji wa Mkataba huu hapaTanzania Serikali imepitisha mwongozo wa pili wa utoaji hufuma za afya ya kinywa na meno 2020 pamoja na kanuni za zebaki 2020, " ameeleza.

Ameongeza kuwa zote hizo zinasitisha utumiaji wa 'Dental Amalgam’kwa kuziba meno ya watoto, wanawake wajawazito na wanaonyonesha na wenye umri wa kuzaa.

Hivyo wameitaka Serikali kukuza kasi ya usambazaji wa taarifa kwa madaktari (sekta ya umma na binafsi)na kwa wananchi (ambao ndio walaji wa huduma hizi).

Swai ameeleza kwamba wananchi wanahaki ya kuchagua adawa ya kuzibia jino ila wanaweza kufanya hivyo kama watakuwana taarifa za kutosha.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TCAR Bernard Kihiyo amesema serikali na wadau wengine wanapaswa kukuza ufahamu kwa jamii kuhusi usitishwaji wa Dental Amalgom ili waweze kuchagua kutumia dawa zisizo na zebaki.

Pia amesema Serikali inatakiwa isitishe matumizi ya Dental Amalgam kwa watu wa makundi mengine ambayo hayajaguswa kwa sasa kama wanawake na wanaume wengine ili makundi yote ya wananchi yaguswe kama vile ilivyofanya nchi ya Garbon ambayo kwa mwaka huu imepitisha kusitishwa kwa Dental Amalgam kwa watu wote.

Awali Katibu Mtendaji wa AGENDA Haji Rehani ameeleza kwamba utumiaji wa dawa zisizo na zebaki kwa kuziba meno yaliyotoboka inawezekana kabisa — nazimekuwazinatumikahata kablaya kupitishwa kwa Mkatabawa Minamata ..

Amesema baadhi ya dawa za kuziba meno ambazo hazina zebaki ambazo pia zimekuwa zinatumika hapaTanzania huku akifafanua ni Zebaki ni sumu ya mfumo wa fahamu ambayo inaweza kuathiri ubongo na mfumo wa neva wa binadamu.

"Tunaweza kutoka kwa mama na kuingia kwa mtoto akiwa tumboni au kupitia maziwa ya mama wakati wa kunyonyesha.Athari nyingine za zebaki ni kutetemeka mwili, ku fubaza uwezo wa kuona na kusikia,kupooza kwa viungo.

"Pia kukosa usingizi na kuongeza kuwa na hasira. Pia zebaki inaweza kuathiri mfumo wa uzazi, inaweza kuathiri mbegu za kiume, madhara wakati wa kuzaliwa mtoto, mimba kutokana matatizo mengine ya kujifungua."

Ofisa Programu Mwandamizi wa AGENDA Dorah Swai (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wakiadhimisha Wiki ya Afrika ya kupinga matumizi ya dawa zenye zebaki ya kuziba meno yaliyotoboka.Kushoto ni katibu Mtendaji wa AGENDA Haji Rehani na Mkurugenzi Mtendaji wa TCAR Bernard Kihiyo(kulia).




 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...