Na Ashrack Miraji Same kilimanjaro

MBUNGE wa Same Magharibi Dk.David Mathayo amesema  michezo  inawajenga vijana kuwa na mahusiano mazuri Katika nyanja mbali mbali na kuweza kutimiza ndoto zao pia  kuachana na vitendo viovu   kama ukabaji na kutumia madawa ya kulevya, bangi na mirungi 

Hayo ameyasema wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa Michuzi Blog kuelekea uzinduzi wa Dk.Mathayo Cup inayotarajia kuanza Novemba 26 katika jimbo la Same Magharibi mkoani kilimanjaro ambapo timu 56 zitakwenda kushiriki mashindo hayo.

Amesema dhamira yake kwa vijana ni kubwa kwani anatamani kuona wanafika mbali na kutimiza ndoto zao hivyo atakuwa nao bega kwa bega katika kuleta maendeleo chanja kwenye jimbo la Same Magharibi sambamba na kuza vipaji vyao.

Dkt Mathayo amesema  pia michuano ya Mathayo Cup ni sehemu ya kumuunga mkono Rais Dk.Rais Suluhu katika sekta za  michezo huku akisisitiza wanaona Rais akifatilia michezo tofauti kwa  ukaribu na kuzipa timu zetu  hamasa katika mashindano ya kimataifa.

"Mimi kama mwakilishi wake katika Jimbo la Same Magharibi nitahakikisha vijana wa Same Magharibi wananufaika katika michezo na shughuli mbalimbali za kiuchumi, " amesema.

Aidha ametumia nafasi hiyo kueleza mambo makubwa ambayo Rais Samia ameyafanya katika jimbo hilo ikiwemo ujenzi wa miundombinu katika sekta ya afya, barabara, elimu pamoja na kuboresha maeneo mengine kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

"Niwaombe  wananchi wa Jimbo  langu kuendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassani kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuleta maendeleo kwenye jimbo letu na Taifa."



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...