Timu ya Netiboli ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania- TPA “ Bandari Queens “ imeendelea kutembeza vipigo kwa timu pinzani Katika Mashindano ya ligi daraja la pili Taifa yanayofanyika Mkoani Katavi, ikiandikisha rekodi ya kushinda Michezo 7 mfululizo hadi sasa.

Bandari Queens inayonolewa na Kocha Judith Ilunda imekuwa mwiba kwa Timu pinzani Katika Mashindano hayo ambapo imefunga jumla ya magoli 379 na kuwa Timu gumzo.

Meneja wa timu hiyo Fatma Mwinjaka anasema wanajivunia kikosi bora na maandalizi Kabambe waliyopewa na Menejimenti ya TPA kuelekea Mashindano haya hivyo imani yao ni kutwaa ubingwa na kupanga ligi daraja la kwanza Taifa.

Kikosi cha Bandari Qeens kina Nyota wakongwe na chipukizi, wakiongozwa na Mfungaji wao mkongwe Neema Mwahu , Mwenye umri wa miaka 58 pamoja na Nahodha wao Irene Mitava.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...