Na Mwandishi Wetu, Pwani

JUMUIYA ya Wafanyabiasha nchini (JWT) imeanza ziara ya kikazi ya kusikiliza kero za wafanyabishara katika wilaya zote za mkoa wa Pwani.

Lengo la ziara hiyo ni kusikiliza kero za wafanyabishara, wenye viwanda na kampuni ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu na kuepuka changamoto ikiwamo migomo ya mara kwa mara.

Mwenyekiti wa JWT, Hamis Livembe, akiongozana na viongozi wengine mapema leo wamewasili ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani na kufanya mazunguzo na Katibu Tawala, Rashid Mchatta kabla ya kuanza mikutano yao.

Livembe amesema Rais Samia anawapenda wafanyabishara ndio sababu amewaagiza wasikilize kero zao ili kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

Amesema wafanyabishara wakiungana wanaweza kujisemea na kumaliza kero zao bila kufunga biashara wala kufanya vurugu hivyo ni muhimu kujitokeza kwenye mikutano hiyo.

Naye Mchatta ameipongeza jumuiya hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuisaidia serikali kusikiliza kero hizo nchi nzima na kuzifilisha kwenye mamlaka husika.

"Niwasihi tu viongozi wa JWT msiache kuwaelimisha wafanyabishara umuhimu wa kulipa kodi pamoja hayo wazingatie tahadhari za mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini," amesema.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...