Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Bideko, amekutana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), CPA. Hosea Kashimba, Bungeni jijini Dodoma.
PSSSF, ni miongoni mwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
CPA. Kashimba alipata fursa ya kumpongeza Dkt. Biteko kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo Agosti 30, 2023 na kula kiapo Septemba 1, 2023.
Pia CPA. Kashimba alitumia fursa hiyo kujitambulisha ikiwa ni pamoja na kumueleza utekelzaji wa majukumu ya Mfuko kama yalivyoainishwa kwenye Sheria namba 2 ya mwaka 2018 iliyoanzisha PSSSF, ambayo ni pamoja na Kuandiskisha Wanachama, Kukusanya Michango, Kuwekeza na kulipa Mafao.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Bideko, akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, ofisini kwa Naibu Waziri Mkuu kwenye ofisi za Bunge jijini Dodoma, Novemba 3, 2023. PSSSF iko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.


Dkt. Bioteko (kulia), akiwa kwenye mazungumzo na ujumbe wa PSSSF ulioongozwa na CPA. Kashimba. Wengine pichani ni Meneja Uhusiano na Elimu kwa Wanachama, PSSSF, Bw. James Mlowe (wapili kushoto) na Afisa Mkuu wa Uhusiano, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...