Rais wa Romania, Mhe. Klaus Iohannis amewasili Zanzibar kwa Boti ya AZAM na kupokelewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi- Zanzibar, Mhe. Jamal Kassim Ali.
Akiwa Zanzibar, Rais Iohannis atakutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na baadaye kutembelea Mji Mkongwe ambao ni moja kati ya vivutio vikubwa vya utalii duniani. Rais Iohannis ambaye yupo nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku nne ataondoka nchini tarehe 19 Novemba 2023.
Akiwa Zanzibar, Rais Iohannis atakutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na baadaye kutembelea Mji Mkongwe ambao ni moja kati ya vivutio vikubwa vya utalii duniani. Rais Iohannis ambaye yupo nchini kwa ziara ya kitaifa ya siku nne ataondoka nchini tarehe 19 Novemba 2023.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...