Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi,akizungumza wakati akifungua kongamano la vijana la kisayansi lililofanyika Mkoani Morogoro.

 

Na; Mwandishi Wetu, MOROGORO

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amewataka vijana nchini kuwa wazalendo na kuzingatia maadili ili kuwa taifa bora sasa na baadae.

Mhe. Katambi ametoa rai hiyo wakati akifungua kongamano la vijana la kisayansi lililofanyika Mkoani Morogoro kwa lengo la kujadili na kupata elimu kuhusu mambo mbalimbali yanayohusu mapambano dhidi ya UKIMWI.

“Vijana wana mchango mkubwa katika ujenzi wa taifa na wanaweza kutoa mchango mkubwa zaidi iwapo mtafanya shughuli zenu kwa kuzingatia uzalendo, weledi na maadili,” amesema.

Aidha, ameeleza kuwa Utafiti wa Viashiria vya UKIMWI mwaka 2016/2017 nchini, umeonyesha kuwa moja ya makundi yaliyo nyuma katika kufikia malengo ni vijana huku wengi wenye umri mdogo hawajui hali zao za maambukizi ukilinganisha na watu wenye umri mkubwa, hali inayosababidha vijana wenye virusi vya UKIMWI kutoanza dawa za ARV mapema.

Vile vile, Mhe. Katambi ametoa rai kwa vijana nchini kujitokeze kwa wingi katika huduma za upimaji wa VVU kwa hiari sambamba na kupiga vita mmomonyoko wa maadili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...