Katika kuadhimisha Siku ya Wanaume Duniani, Benki ya CRDB imefanya semina ya siku moja kwa wafanyakazi wake wanaume ili kuwajengea uwezo katika masuala ya kisaikolojia, kimwili na kijami.

Semina hiyo iliendeshwa na madaktari pamoja na wanasaikolojia, na kufanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam. 

Licha ya kuwajengea wafanyakazi kusimamia mambo yao binafsi, warsha hiyo imelenga kuongeza morali na kuwatia moyo wa kujituma zaidi kila wanapowahudumia wateja ili kukidhi mahitaji na matarajio yao ya kifedha.

Siku ya Wanaume Duniani huadhimishwa kila ifikapo Novemba 19 ya kila mwaka ili kutoa nafasi kwa wanaume kujadili maendeleo yao binafsi pamoja na ya familia zao na kutafuta suluhu ya changamoto wanazokabiliana nazo.

Zikiwa zimebaki siku mbili kabla ya kilele cha maadhimisho hayo, wafanyakazi wa Benki ya CRDB wamepitishwa kwenye mada kadhaa ikiwamo afya ya akili, afya ya uzazi, familia na malezi pamoja na saikolojia ya jamii.

Mjadala huo umelenga kuwajengea uwezo wa kurahisisha maisha yao ndani ya ndoa, maisha binafsi pamoja na jinsi wanavyochangamana na jamii bila kusahau maisha yao wakiwa kazini.
Mtaalamu wa Masuala ya Saikolojia nchini, Dkt. Ellie Waminian akizungumza katika semina ya siku moja kwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wanaume ili kuwajengea uwezo katika masuala ya kisaikolojia, kimwili na kijami, iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB ambaye ni Afisa Mkuu wa Fedha, Fredrick Nshekanabo akizungumza katika semina ya siku moja kwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wanaume ili kuwajengea uwezo katika masuala ya kisaikolojia, kimwili na kijami, ikiwa ni sehemu kuadhimisha Siku ya Wanaume Duniani, iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam. 
Afisa Mkuu wa Uendeshaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwile akizungumza katika semina ya siku moja kwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wanaume ili kuwajengea uwezo katika masuala ya kisaikolojia, kimwili na kijami, ikiwa ni sehemu kuadhimisha Siku ya Wanaume Duniani, iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam. 
Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Timothy Fasha akizungumza katika semina ya siku moja kwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wanaume ili kuwajengea uwezo katika masuala ya kisaikolojia, kimwili na kijami, ikiwa ni sehemu kuadhimisha Siku ya Wanaume Duniani, iliyofanyika katika makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam. 









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...