Afisa uhusiano Aika Swai kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)akitoa elimu kwa wateja waliotembelea katika banda hilo juu ya namna ya uapatikanaji wa leseni Kijiditi katika viwanja vya Shekh Amri Abeid Jijini Arusha kwenye maonyesho ya huduma za kifedha kitaifa
Afisa Mwandamizi mkuu,TCRA Semu Mwakyanjala TCRA akitoa elimu kwa wateja waliotembelea katika banda hilo juu ya namna ya uapatikanaji wa leseni Kijiditi katika viwanja vya Shekh Amri Abeid Jijini Arusha kwenye maonyesho ya huduma za kifedha kitaifa
Na.Vero Ignatus,Arusha
Mamlaka ya mawasiliano Tanzania inaendelea kuhamasisha upatikanaji wa Leseni Kijitali kupitia mfumo wa lango kuu la utoaji wa huduma za mawasiliano (Tanzanite Portal) leseni zinazotoa huduma ni 2,518,Watoa huduma za mawasiliano wapo 1,531,Vyeti vya wanaothibitisha ubora wa vifaa vya mawasiliano wapo 2,157(type Aproval)
Semu Mwakyanjala ni Afisa Mwandamizi,TCRA Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Arusha katika wiki ya huduma za Fedha Kitaifa alisema kuwa mfumo huo utamrahisishia mtoa huduma kuhuhisha leseni zao kirahisi kupitia mfumo huo ambapo amewasisitiza wananchi kupata huduma kwa mtu aliyesajiliwa na TCRA.
Mwakyanjala amesema katika hali ya kuendeleza huduma za kidijiti nchini TCRA inatoa rasilimali hadimu za masafa, namba na kikoa bure kwa wabunifu kwaajili ya majaribio ya tafiti zenye tija,
pia TCRA imeanzisha klabu za kijiditi Tanzania kuanzia shule za awali,msingi ,sekondari vyuo vikuu ili kukuza ustadi wa kijiditi na teknolojia miongoni mwa wanafunzi.
"Kama wewe ni fundi na unajishughulisha na nanukarabati wa vifaa vya mawasilianao kama vile simu unapaswa kuwa na leseni ya TCRA ni rahisi kujisaili kupitia www tanzanite. tcra. go. tz ili ili kupata leseni yako" alisisitiza Mwakyanjala.
Ameaniasha shughuli katika klabu hizo ni pamoja na kujumuisha mafunzo ya program mbalimbali zinazohusu teknolojia za kijiditi , ubunifu uvumbuzi kwa njia ya kompyuta , kujifunza jinsi ya kutumia programu za zana za kijiditi na miradi ya kiteknolojia inayohisiana na masuala ya kijamii na kiuchumi.
"Kwenye klabu hizi vijana wanafunzi wanaweza kunufaika kwa fursa za semina zinazotolewa na wadau mbalimbali wa sekta, pia vigezo vinaweza kubadilika kulingana na klabu,shule au chuo, na mara nyingi tunashauri wanafunzi wajiunge kwenye klabu hizi kwa hiari na inaweza kuwasiliana na mwalimu wa jukumu la. Klabuau kiongozi wa klabu"
Aidha ameainisha njia ambavyo TCRA inachukuabili kuongeza ushiriki wa wanafunzi katika klabu za kijiditi ni pamoja na kuandaa kitabu cha kuanzisha na kuratibu klabu , kushirikiana na wadau wakiwemo wadau wa elimu kuhakikisha uanzishaji wa klabu pamoja na kutoa elimu.
"Wananchi mtumiaji wa husuma za. Mawasiliano za simu, intaneti , utangazaji naposta kumbuka mara zote kutumia huduma ya watoa hiduma ya liosajiliwa na TCRA , huduma iliyosajiliwa inakupa hakikisho lamusalama na ulinzi wanhaki zako za huduma" alisema
Sambamba na hayo amewata wananchi kutambua kuwa udhalilishaji mtandaoni ni kosa la jinai,hivyo amewataka kutoa taarifa kupitia mfumo wa mrejesho kwenye ukurasa wa mtandao husika,pia amewataka kutokuchapisha ma
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...