NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ametembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwenye Maadhimisho ya 3 ya Wiki ya Huduma ya Fedha Kitaifa kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Novemba 22, 2023, ili kujionea jinsi wanavyowahudumia wananchi.

Mhe. Majaliwa alipokelewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhanisi Cyprian Luhemeja na kupitishwa kwenye mabanda yaliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, WCF ikiwemo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, alimueleza Waziri Mkuu kuwa WCF na mifuko mingine ya hifadhi ya jamii, inashiriki katika Maadhimisho hayo yenye kauli mbiu isemayo, "Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo Kiuchumi", ili kutoa elimu kwa umma kuhusu hifadhi ya jamii lakini pia elimu ya matumizi sahihi ya fedha.

Alisema, WCF, inahudumia wafanyakazi wanaoumia au kuugua wawapo kazini.

“Ni muhimu sana kwa waajiri kuwekeza katika afya za wafanyakazi kwani binadamu anaweza kupatwa na changamoto wakati wowote na hapo ndipo unakuja umuhimu wa waajiri kujisajili ili kuwawekea kinga ya kipato wafanyakazi wao wanapopatwa na changamoto wanapotekeleza majukumu ya kazi walizoajiriwa kuzifanya.” Alisema.

Akieleza kuhusu jinsi wanavyohudumia wananchi wanaotembelea kwenye banda hilo, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano WCF, Bi. Laura Kunenge, alimueleza Waziri Mkuu kuwa, wanatoa elimu ya fidia kwa wafanyakazi, lakini pia Mafao yanayotolewa na Mfuko kwa Mfanyakazi anayeumia au Kuugua kutokana na kazi na endapo atafariki, basi Mfuko unabeba jukumu la kuwalipa fidia wategemezi wake.

“Kwa hivyo kupitia mafao tunayotoa, tunapunguza umasikini katika jamii yetu.” Alisema.

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (wapili kulia), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Profesa Joyce Ndalichako (wakwanza kulia), Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu), Mhandisi Cyprian Luhemeja, (wapili kushoto), wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Laura Kunenge, wakati akieleza huduma zitolewazo kwenye banda la Mfuko huo Novemba 22, 2023.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Profesa Joyce Ndalichako, akiteta jambo na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhandisi Cyprian Luhemeja
Elimu ya fidia ikiendelea kutolewa kwa wananchi waliofika banda la WCF.
Elimu ya fidia ikiendelea kutolewa kwa wananchi waliofika banda la WCF.
Mwananchi akisikilzia kwa makini, maelezo yaliyokuwa yakitolewa na wafanyakazi wa WCF kuhusu huduma za Mfuko huo.
Picha ya pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...