Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako,akizungumza kwenye kikao cha Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Watumishi waliopo chini ya Ofisi yake kilichofanyika leo Novemba 11,2023 jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amesema Ofisi hiyo pamoja na Taasisi zake zitaendelea kutekeleza majukumu kwa ufanisi na kuwahudumia wananchi kwa wakati.

Prof.Ndalichako ameyasema hayo Novemba 11, 2023 kwenye kikao cha Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na Watumishi waliopo chini ya Ofisi yake kilichofanyika katika ukumbi wa PSSSF jijini Dodoma.

Aidha, Waziri Ndalichako amesema katika kikao hicho kitawasaidia kukumbushana watumishi wajibu wao pamoja na kutengeneza ushirikiano na uhusiano mzuri katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu tutaendelea kuwa timu imara ambayo lengo letu ni kuhakikisha kwamba majukumu ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Taasisi zilizopo chini yake yatatekelezwa kwa ufanisi wa hali ya juu,” amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...