Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Dkt. Hussen Omary amewaagiza wamiliki wa mashamba na viwanda vinavyochakata chai nchini kuzingatia malipo ya wafanyakazi wadogo katika viwanda hivyo ili kuendeleza zao la chai nchini.

Maagizo hayo ameyatoa leo katika hafla ya uzinduzi wa mnada wa zao la chai uliofanyika Dar es salaam wenye lengo la kukuza na kuendeleza zao la chai nchini ambapo Dkt Hussen ametumia hafla hiyo kueleza umuhimu wa mkulima mdogo katika kilimo hivyo ni budi kwa wamiliki wa mashamba kuzingatia masilahi ya wakulima hao.

Amesema hadi kufikia mwaka 2030 malengo ya Serikali ni kutengeneza ajira zaidi ya milioni tatu kupitia sekta ya kilimo ususani kwenye zao la chai

Imeelezwa kuwa kufanyika kwa mnada huo hapa nchini kutasaidia kuinua soko la chai ndani na nje ya mipaka.

Hivi ni mara ya kwanza kufanyika kwa mnada huo wa chai nchini ambapo unatajwa kusaidia kulitangaza zao la chai kwenye soko la nje.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...