Na Mwandishi Wetu 

UONGOZI wa Kampuni ya Franone  Mining  and Games limetd  inayojishughulisha na uchimbaji madini ya vito ( Tanzanite) imeungana na watanzania wengine na Serikali katika kuchangia mahitaji mbalimbali ikiwemo  chakula Kwa  waathirika wa mafuriko wilayani Simanjiro mkoani Manyara .

Akizungumza na waandishi na waandishi wa habari baada ya kutoa msaada huo,  Meneja Mkuu wa kampuni hiyo Vitus Ndakize amesema  wameguswa  na tukio hilo hivyo wao kama wawekezaji waliowekeza kwenye uchimbaji wa madini  wameona wachangie watanzania wenzao ambao wamepatwa na majanga hayo Kwa kutoa bidhaa mbalimbali pamoja na chakula.

Amesema miongoni mwa vitu ambavyo wamechangia na kukabidhi Kwa mkuu wa Wilaya hiyo  Dkt. Seleman Selela ni pamoja na magunia 200 ya mahindi , maharagwe gunia 40 ,Sukari mifuko 20, na mafuta kantoni 40 za lita moja ambapo jumla ya msaada wote ugharama zote ni Sh.milioni 31.

Vitus ameongeza kuwa wao kama Kampuni wamekabidhi mahitaji hayo hivyo viongozi husika ndio wataona wanagawaje  lakini wameelekeza kwenye kata mbili ambazo ni ,kata ya mto wa tembo , na kata ya shambalai.

" Kampuni tumetoa kwa ujumla ila uongozi wa Wilaya wao ndio wanajua namna watakavyogawanya  chini ya usimamizi wa Mkuu wa Wilaya na Mbunge wa Jimbo husika."

Pia Vitusi amewashauri  wadau kuendelea kujitoa kwa hali na mali na kwamba wakati mwingine majanga kama hayo yanapotokea watu wanakuwa hawajajipanga, hivyo ni vema kujitoa kusaidia wenye uhitaji.

Ametoa mwito kwa watanzania kuendeleza umoja kama watanzania na hasa yanapotokea majanga kama hayo  huku akiipongeza  Serikali hasa ngazi ya Wilaya imefanya kazi kubwa  kuhakikisha waathirika hao wanapata mahitaji ya kibinadamu.

"Na  kwasababu Serikali haiwezi kufanya kila kitu kwa hiyo na sisi kama wadau tumeona tutoe mchango wetu  ili  kuunga mkono jitihada za Serikali kuhudumia watu wake."

Akimzungumzia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ukatisha ziara na kurudi haraka nchini kuungana na watanzania wengine baada ya kutokea mafuriko ya matope Hanang,  Vitusi amesema Rais Dkt Samia ameendelea kuthibitisha yeye ni mtu wa watu na anawapenda wananchi.

Ameongeza Rais Dk.Samia  ni mama anayejali watu wake  na aliamua kukatisha ziara yake ya kikazi ili kuja nyumbani na kuwaona wananchi wake waliokumbwa na mafuriko hayo yaliyosababisha vifo , majeruhi na uharibifu wa mali.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Simanjiro mkoani Manyara Christopher Ole Sendeka ameipongeza kampuni ya Franone Mining and Games kwa kuwachangia waathirika wa mafuriko hayo.

Ole Sendeka amesema kampuni hiyo imekuwa msaada mkubwa kwenye jamii kwani hivi karibuni wakati wa ukame ilisaidia chakula kwenye shule mbili zilizokuwa zinakabiliwa na uhaba wa chakula zilizopo kata ya Naisinyai

Awali Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Asia Ngaliwason ameishukuru kampuni hiyo  na kuwahakikishia  msaada huo utafika kwa wahusika waliokumbwa na mafuriko

Ameongeza kuwa waliokumbwa na mafuriko ni watu 126 na watapata msaada huo katika kata za shambarai na kata ya msitu wa Tembo kwenye kaya 49.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...