Na Said Mwishehe-Michuzi TV-Chato

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Abdulurhaman Kinana ameeleza sababu za msingi ambazo zinasababisha Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kusifiwa na sababu kubwa ni namna ambavyo ameendelea kutekeleza miradi ya maendeleo na hakuna mradi  hata mmoja ambao umesimama.

Kinana ameyasema hayo leo Desemba 12, 2023 mbele ya wananchi wilayani Chato mkoani Geita wakati  Mbunge wa Jimbo la Chato Dk.Merdard Kalemani akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani katika kipindi cha miaka miwili na nusu.

"Rais Samia Suluhu Hassan anafanya kazi nzuri na wakati mwingine nimeona zimeanza kauli wanasema mbona mnamsifu sana  Rais lakini lazima tukubaliane wakato wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kusema hivi kuongoza ni kuonesha njia.

" Ukiwa  na kiongozi mzuri , msikivu, mwenye kushirikiana na wenzake wakapanga na mambo yakawa kwanini tusimsifu , lazima tumsifu maana ndio anayetuongoza .Huko nyuma Baba wa Taifa tulikuwa tunasema zidumu fikra za mwenyekiti lakini fikra hazikuwa za Mwenyekiti ni za Chama cha TANU na CCM...

"Kwasababu gani? Ndio kiongozi wetu anafanya kazi nzuri.Rais Samia kwa muda mfupi sana amefanya kazi kubwa sana,  ukimwambia Mkuu wa Mkoa hapa asimame aeleze fedha zilizoletwa katika mkoa huu katika kipindi cha miaka 20 iliyopita basi nina hakika fedha zinazotolewa kipindi cha Rais Samia inaweza kuwa mara 10, " amesema.

Amefafanua jana alikuwa  Mkoa wa Kagera ambapo ameelezwa Rais Samia amepeleka fedha Sh.bilini 260 , lakini kuna wakati alienda Rukwa ambapo aliambiwa amepewa  Sh.bilioni 256  na Geita wamepewa zaidi ya Sh.bilioni 300 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

"Nanyi ni mashahidi chini uongozi wake mapato ya nchi yameongezeka , chini ya uongozi wake miradi yote mikubwa iliyoanzishwa na Hayati Dk.John Magufuli hakuna uliosimama .

"Hapa Chato kuna mradi umesimama?Miradi yote inaendelea na mingine imekamilika .Kila kitu kinaendelea.Dk.Magufuli aliacha ujenzi wa reli ya kisasa(SGR) aliacha Bwawa la kufua Umeme la Mwalimu Nyerere na sasa shughuli zinaendelea .

"Taarifa zilizopo umeme kutoka katika bwawa lile mwezi wa kwanza megawati 250 zitaingia kwenye gridi ya Taifa.Hivyo changamoto ya umeme itaendelea kupungua kadri megawati za umeme kutoka Bwawa la Mwalim  Nyerere zinapoingia kwenye gridi ya Taifa.




 

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...