Na John Walter-Manyara
Juhudi za kuwaokoa watu waliokwama kwenye
Matope zimeendelea Vijiji vya Katesh na Gendabi wilayani Hanang mkoani
Manyara baada ya Mafuriko kuyakumba maeneo hayo na kusababisha vifo vya
watu 47 na wengine 85 kujeruhiwa.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Queen Sendiga watu zaidi wanahofiwa kufukiwa na matope baada nyumba na makazi yao kusombwa na mafuriko na maporomoko ya udongo kutoka Mlima Hanang'.Eneo kubwa lililoathiriwa na mafuriko hayo ni kata ya Gendabi na Katesh ambapo ndipo makao makuu ya Wilaya ya Hanang'.
Nyumba
za watu zimezingirwa na mafuriko na miti iliyosombwa na mafuriko kutoka
sehemu ya Mlima Hanang yamesababisha barabara ya Katesh kwenda Singida
kushindwa kupitika kwa muda.
Wakazi wa Hanang' wamesema hawajawahi kushuhudia hali kama hiyo na kwamba kwao hilo ni janga kubwa.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan ametuma
salamu za pole kufuatia tukio hilo na kuzitaka mamlaka zote zihamishie
nguvu wilayani Hanang kutoa msaada wa haraka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...