Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Disemba 15, 2023 amewasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ivato uliopo Antananarivo nchini Madagascar na kupokelewa na Waziri Mkuu wa Madagacar, Christian Ntsay.

Mheshimiwa Majaliwa kesho Disemba 16, 2023 atamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye sherehe za kumwapisha Rais wa nchi hiyo, Andry Rajoelina kwenye uwanja wa Mahamasina Barea Stadium.

Mheshimiwa Rajoelina ameshinda nafasi hiyo kwa muhula wa tatu kwa asilimia 58.9 ya kura zilizopigwa akifuatiwa na Siteny Randrianasoloniaiko ambaye alipata kura 14.39.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...