Na Chalila Kibuda,Michuzi TV

Serikali imesema kuwa mambo yanayoendelea katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT) hajui chochote kutokana na chama hicho hakijapeleka malalamiko yeyote.

Hayo ameyasema Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako siku moja baada ya chama hicho kutoa taarifa katika mitandao ya jamii kuhusiana na kustisha kufanyika kwa maadhimisho ya miaka 30 kutokana kutokuwepo kwa Mgeni Rasmi Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Prof.Ndalichako amesema Rais kutokuwepo sio ndio kufanya maadhimisho hayo kustisha na taratibu zilizotumika ya kustisha maadhimisho sio sahihi.

Amesema kuwa tarehe zilizokuwa zinapangwa zilikuwa zikiingiliana na majukumu mengine ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan hivyo walitakiwa kupanga tena na sio kupisha ujumbe katika mitandao ya Jamii.

"Serikali hatuna taarifa yeyote juu ya kinachoendea kwenye Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kuwa kuna migogoro hiyo migogoro ndio nasikia hapa lakini Serikali hatuna taarifa hizo.

Amesema maombi yao ya kutaka mgeni Rasmi yalikubaliwa lakini CWT kwa Mwezi wa 10 yalikubaliwa wakaomba kusogeza muda na kusogeza kutokana majukumu ya Rais yaliingiliana na majukumu mengine.

Aidha amesema Rais anathamini kazi ya CWT na Walimu kwa kazi zao na kuwa karibu katika kutatua changamoto zao.

Amesema kubadiika kwa tarehe kwa Rais na majukumu yake inakuwa changamoto ambapo sio nia yake ya kutotaka kuwa mgeni rasmi.

Amesema kuwa walimu wote nchini na CWT itaendelea kushirikiana hatua kwa hatua pamoja na kuendelea kuboresha mazingira walimu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Chama cha Walimu Tanzania  (CWT) kusitisha maadhimisho ya miaka 30 ya Chama hicho kwa kutoa taarifa Mtandaoni jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...